Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Counterpoint, simu za Xiaomi zimeongeza sehemu kubwa ya soko lake nchini India katika robo tatu ya mauzo yake katika mwaka huu na kubakisha pengo dogo na simu za Samsung.
Xiaomi zimeuza kwa asilimia 22 ya simu zote zilizouzwa nchini India katika robo tatu ya 2017 ambapo robo tatu ya mwaka uliopita iliuza kwa asilimia sita pekee. Hii inamaanisha mauzo ya simu za Xiaomi yamepanda sana kulinganisha na Samsung ambao wamebaki katika asilimia 23 ya mauzo ya robo tatu kwa mwaka jana na mwaka huu pia.
Kupanda kwa mauzo ya Xiaomi kumechagizwa sana kwa ubora wake na bei yake nafuu ambapo kwa soko la India ni muhimu na huzingatiwa sana. Takwimu zinaonesha kwamba Samsung itahitaji mabadiliko fulani ikiwa inataka kubaki juu kwenye soko la India, vinginevyo katika robo ya nne ya mwaka huu Xiaomi inaweza kuongoza mbele ya Samsung.
Xiaomi ni kampuni ya kichina yenye makao yake makuu huko Beijing inatajwa kama kampuni ya tano kwa uzalishaji wa simu duniani. Mbali na kutengeneza simu pia inatengeneza Laptop, vifaa vya elektroni na App mbalimbali.
Majina ya simu za Xiaomi yana familia mbili moja Mi na nyingine Mi note, ambapo simu za karibuni kutoka familia hizo ni Mi Note 3,Mi Note 2, Mi 6, Mi 5c na nyingine nyingi.
Kampuni Xiaomi Inc ilianzishwa April mwaka 2010 na simu janja yake ya kwanza ilitolewa mwaka 2011. Mwanzilishi wake anajulikana kama Lei Jun na kwa mujibu wa Forbes ni tajiri namba 23 duniani.