Biashara ni ushindani na ukitaka kuweza kupenya soko na bidhaa yako kuuzika kwa wingi basi ni muhimu kuangalia kitakachowavutia walaji/wateja. Sasa makampuni kadha wa kadha wameweza kurudisha kwenye ramani ya ushindani lakini swali ambalo tunajiuliza ni ni ipi kati ya zile zinazoweza kukunjika (inayoweza kukunjika) zitauzika kirahisi?
Xiaomi anatazamia kuingia kwenye ushindani wa simu janja inayoweza kukunjika kusumbua wapinzani wake Samsung, Huawei katika hali ya “Akili ya kibiashara” kutokana na bidhaa yake inayoweza kukunjika anatazamiwa kuizindua kati ya mwezi Aprili na Juni mwaka huu.
Rununu ya Xiaomi ambayo inaelezwa kuitwa Mi Fold na nyingine kuitwa Mi Flex itakuwa inauzwa nusu bei ya Galaxy Fold na Huawei Mate X ambazo ni $1,980|Tsh. 4,554,000 na $2,600Tsh. 5,980,000 mtawaliwa huku hiyo ya Xiaomi ikielezwa kuuzwa kuanzia $999|Tsh. 2,297,700. Mbali na hapo simu hiyo inaelezwa kuwa Snapdragon 855 SoC, upande wa RAM ina GB 10.
Xiaomi au niseme “Mchina” anajua kuharibu soko ili kufanya bidhaa zake ziuzike kiulaini. Sasa ndio hapo utakapoamua ipi ununue kulingana na uwezo wako pamoja na vigezo mbalimbali.
Vyanzo: GSMArena,