Kampuni ya Microsoft imetangaza kuwa kwa sasa kuna karibu kompyuta milioni 700 zilizounganishwa na Windows 10.
Mkurugenzi Mtendaji wa Microsoft, Satya Nadela alisema hayo katika mkutano wa wanahisa wa kila mwaka kwamba kuna zaidi ya kompyuta milioni 600 zilizounganishwa na Windows 10. Microsoft Windows ndio mfumo endeshi maarufu zaidi duniani wa kompyuta na hakuna dalili yoyote ya kupungua kwa matumizi yake kwa muda wa karibuni.