WhatsApp itaacha kufanya kazi kwa mamilioni ya watumiaji wa simu janja kadhaa mwishoni mwa mwaka huu kampuni hiyo imethibitisha.
Simu ambazo zitakumbwa na anguko hilo ni zile za mfumo endeshi wa BlackBerry OS, BlackBerry 10, Windows Phone 8.0 na chini ya hapo. Muda wa mwisho uliotolewa awali ulikuwa ni Juni 30 2017 lakini mmiliki wa Facebook ambaye pia ni mmiliki wa whatsApp alisogeza mbele mpaka Desemba 31, 2017.
Wakati huohuo simu za Android za toleo 2.3.7 na chini ya hapo zitaacha kupata masahihisho ya WhatsApp mpaka mwaka Februari 1 2020. Aidha simu ya Nokia S40 nayo imesogezwa mpaka Desemba 31, 2018.
kwa mujibu wa taarifa kutoka WhatsApp wakati wowote kuanzia sasa WhatsApp itaacha kufanya kazi katika simu zilizotajwa.
Orodha kamili ya simu janja zitakazokosa WhatsApp.
>Nokia Symbian S60 mwisho kuanzia juni 30, 2017,
>BlackBerry OS na BlackBerry 10 mwisho Desemba 31, 2017,
>Windows Phone 8.0 na chini ya hapo mwisho Desemba 31, 2017,
>Nokia S40 mwisho Desemba 31, 2018,
>Android Version 2.3.7 na chini ya hapo Mwisho Februari 1, 2018.