Waliokuwa wanasubiria WhatsApp Dark Mode hii ni habari njema kwao. Licha ya kuwa moja ya app maarufu zaidi duniani kwa utumaji ujumbe na picha, WhatsApp bado imekuwa ikipata changamoto za kukosa sifa muhimu ambazo zimekuwepo kwa app nyingine pinzani ya Telegram.
Mojawapo ya kipengele muhimu ambacho WhatsApp imekuwa ikikikosa ni kuwa na muonekano wa giza (Dark Mode). Baada ya maombi mengi ya watumiaji wake, WhatsApp imeanza kukifanyia majaribio kipengele hicho kwa watumiaji wa simu za mfumo wa Android.
Wameanza majaribio kwa watumiaji wa Android wanaotumia toleo la WhatsApp la 2.19.82. Hata hivyo kipengele hicho hakitaweza kupatika kwa watumiaji wote kwa kuwa bado kipo kwenye hatua za majaribio (Beta).
Imeelezwa kipengele hiki kilianza kufanyiwa kazi na WhatsApp tangu mwezi wa Septemba 2018 baada ya watumiaji wake kupendelea kuwepo kwa kipengele hicho.
Kuwepo kwa Dark Mode kwa WhatsApp kutasaidia kupunguza matumizi ya Chaji tofauti na ilivyo sasa kwa programu ya WhatsApp.
Kujiunga katika kutumia app ya WhatsApp Beta tembelea hapa -> Google PlayStore WhatsApp Beta