Instagram imetangaza kwamba kwa sasa ina watumiaji bilioni moja duniani kote. Mwezi Septemba mwaka jana (2017) Instagram ilikuwa na watumiaji wapatao milioni 800 ambapo ndani ya kipindi cha miezi sita imepata ongezeko kubwa la watumiaji wake.
Programu tumishi ya Instagram inakadiriwa kuongeza watumiaji milioni 200 kila mwaka. Ongezeko hilo linaelezwa kuchagizwa na kuongezwa kwa vipengele vya stories, GIF na emoji sliders vimewavutia wengi kujiunga na mtandao huo wa kijamii.
Aidha, inaaminika kuwa kipengele kipya cha IGTV kwenye Instagram kutavutia ongezeko kubwa kwa watumiaji wa mtandao huo wa kijamii, kujua undani wa IGTV BOFYA HAPA.
One Comment
Comments are closed.