Google imetangaza rasmi toleo lake kubwa lijalo la Android juma lililopita likiitwa Android 9 Pie.
Toleo hili lipo tayari kwa mageuzi mapya likiwa katika muundo imara na limeanza kupatikana kirahisi kwa watumiaji kwa kupakua kupitia baadhi ya simu za Google Pixel.
Android Pie ni toleo kubwa la tisa la Android na sasa linachukua nafasi ya toleo la mwaka 2017, Android 8 (Oreo).
Toleo hili lina vitu kadhaa vipya, huku msingi wake ukijikita katika kuwezesha na kutambua haraka namna ya kuifanya simu yako ifanye kazi kwa ufanisi zaidi. Undani wa vipengele vilivyopo kwenye Android Pie ni kama ifuatavyo:-
Adaptive Battery
Miongoni mwa sifa mpya ni kishabihishi cha betri (Adaptive Battery) ambacho hung’amua kwa ufanisi, ni programu tumishi zipi unazitumia kwa uchache na hivyo kuzikatia umeme ili kuliwezesha betri kukaa na chaji kwa muda mrefu zaidi.
Adaptive Brightness
Vivyo hivyo, kishabihishi cha mwanga (Adaptive Brightness) kitarekebisha chenyewe mwangaza sahihi kwenye kioo cha simu kulingana na mahali ulipo kwa wakati husika pia kitu gani unachofanya kwenye simu yako.
Slices
Sifa nyingine mpya kabisa katika toleo hili ni kuwapo kwa ‘Slices’, ambapo programu mbalimbali kujisogeza karibu hivyo kuweza kupata kitu unachotafuta kwa haraka.
Kwa mfano, ikiwa unatafuta “Lyft” kwenye Playstore, programu husika itaonyesha pia ‘Slice’ pamoja na programu nyingine maarufu.
Uwezo wa kutafuta kitu
Android Pie pia inaingiza rasmi mfumo mpya wa ‘navigation’. Kazi za vitufe vitatu vya chini havipo tena na badala yake kipo kitufe kimoja tuu ambacho kinaweza kusogea huku na kule.
Mathalani ukipangusa kwa haraka kutokea kitufe cha nyumbani kwa kwenda juu itakupeleka kwenye programu tumishi ambazo umezifungua, ukishikilia kwa sekunde kadhaa kwa kwenda chini utakuwa umewasha kipengele cha Google Assistant.
Pia miito ya ujio wa taarifa fupi imeboreshwa huku mfumo wa sasa ukipanuliwa kwa kuwa na chaguo thabiti za kujibu ujumbe papo kwa papo (smart reply options).
Digital Wellbeing
Simu zitakazohamia toleo la Android Pie pia zitakuwa na kipengelekiitwacho ‘Digital Wellbeing’ ambacho kinahusisha ukurasa wa mwanzo wa kipengele hicho (Dashboard) ukaoonyesha mwenendo wa simu yako:
katika matumizi ya programu tumishi, kuweka muda maalum (App Timer) kuzuia matumizi kupita kiasi (kuzuia uraibu), ‘Wind Down’ ambacho kitawasha taa usiku na kutokusumbua kwa kioo kubadilika rangi na kuwa kama ya kijivu ili kutoendelea kutumika kupita kiasi kwa simu wakati wa kulala.
Volume Slider
Pia kuna mabadiliko ya ishara ya kupunguza/kuongeza sauti ambapo sasa itapatikana upande wa kulia wa simu yako badala ya juu pale unabobonyeza Batani ya sauti kwa ajili ya kupunguza au kuongeza sauti.
Muonekano wa simu kuzungukazunguka
Kwenye Android 9 sasa utaweza kuona alama ya kuonyesha kuwa umefunga ili isizungukezunguke utakiona upande wa juu kabsa kama kielelezo kuwa kipengele hicho kinafanya kazi yake.