Umoja wa Ulaya (EU) umekuwa ukijaribu kwa karibu muongo mmoja sasa kuwataka wtengezaji wa simu janja kukubali kwa hiari yao kuuza gharama zisizopishana.
Hata hivyo, jitihada hizo hazijafanikiwa na sasa, tume ya umoja huo ipo mbioni kutumia nguvu yake kisheria kuhakikisha kuwa jambo hilo linatekelezwa mara moja.
Kutokana na kusuasua kwa mpango huu wa hiari, muda si mrefu tume itaanza kutathmini athari ili kujua gharama na faida za kuchagua mifumo mingine~Bi. Margrethe Vestager-Msimamizi Mkuu wa Ushindani Kibiashara kutoka EU.
Kwa sasa gharama za kununua simu zimekuwa zikipanda kila litokapo toleo jipya la simu janja hivyo kusababisha watu wengi kushindwa kumudu kuzinunua.
Simu nyingi zilizozinduliwa miaka miwili iliyopita gharama zake zimekuwa juu sana hivyo watumiaji wengi kushindwa kubadili simu zao za zamani kwa kununua simu mpya.