Kituo cha mawasiliano ya intaneti cha Uchina CNNIC kimetoa ripoti kuhusu hali ya maendeleo ya Intaneti ya nchini humo.
Ripoti hiyo imeonyesha kuwa, hadi mwezi Juni mwaka 2018, idadi ya watumiaji wa intaneti milioni 802, ambalo ni ongezeko la watu milioni 29.68 katika nusu ya kwanza ya mwaka huu.
Idadi ya watumiaji wa intaneti kupitia simu za mkononi imefikia milioni 788, ambayo imechukua asilimia 98.8 ya watumiaji wa intaneti nchini China.
Mafanikio hayo yamechagizwa na nini?
Inaelezwa kuwa ujenzi wa miundo mbinu ya mtandao wa intaneti umeboreshwa, sera ya kupunguza gharama na kuongeza kasi ya intaneti imetekelezwa kwa umadhubuti na kuhimiza ongezeko la matumizi ya teknolojia hiyo kwa kupitia simu za mkononi, kompyuta, n.k.