Kama umekuwa mfuatiliajo mzuri wa simu janja zinazobeba jina la Nokia utakubaliana nami kuwa wanaimarika kila mara wanapotoa bidhaa mpya sokoni; saa chache zijazo wanatazamiwa kuzindua Nokia 9.
Jumapili ya Februari 24 2019 kwenye onyesho la MWC19 litakalofanyika huka Barcelona-Uhispania. Simu hiyo inaelewzwa kuwa na mengi mazuri hasa ubora wa picha na ukizingatia kuwa na kamera 5 upande wa nyuma.
Wakati watu wengi duniani kote wakisubiri kuweza kufahamu sifa inazobeba Nokia 9 PureView tayari vionjo ya uwezo wa kamera zake umeweza kubainika kulingana na picha ambacho imepigwa kwa kutumia simu husika kitu ambacho kimezua gumzo kuhusiana na ubora wa kamera zake zipatazo tano (5) kwa idadi.
Sifa za Nokia 9 Pureview
- RAM ya GB 6
- Diski uhifadhi wa GB 128
- Haipati shida ikilowa maji kidogo (waterproof – IP67)
- Ukubwa wa inchi 5.99 (2K OLED)
- Betri la mAh 3,320
Bei ni za kimarekani dola 699 ambazo ni takribani Tsh Milioni 1.6 kwa bei ya kuagiza (ughaibuni) lakini pia imeelezwa kuwa rununu husika haitakuwa na mahali pa kuchomekea spika za masikioni kitu ambacho kimekuwa kikifanywa na makampuni mengi tuu.
Vyanzo: GSMArena, News 18, The Verge
One Comment
Comments are closed.