Kwa taarifa zilizotoka hivi karibuni zinasema kuwa Twitter wapo mbioni kutumia mtindo wa kulinda ujumbe wa watumiaji wake wa mazungumzo yao yanakuwa yanaweza kusomwa kati ya watu wawili tu.
Utaratibu huo (end-to-end) hufanya mazungumzo yote yanayofanywa na watu wawili kubaki kuwa siri bila ya kuweza kuingiliwa na mtu wa tatu.
Mjuzi wa kuandika programu mwenye jicho la Tai, Bi. Jane Manchun Wong pamoja na mitandao mbalimbali amegundua hilo kupitia majaribio na uchunguzi alioufanya kwenye programu ya Twitter kwenye simu za Android.
Mwaka 2016, Edward Snowden alimwomba Mkurugenzi Mtendaji wa Twitter, Bw. Jack Dorsey kuwa na uwezekano wa kulinda mawasiliano kati ya wale wanaowaliana (end-to-end encryption) kwenye Twitter au uwepo na utaratibu wa ujumbe kufutika pale tu muhusika aliyetumiwa atakapousoma.
Ombi la Snowden lilijibiwa na Mkurugenzi huyo kwamba inawezekana na watafikiria ushauri wake. Twitter inayojulikana sana kwa alama yake ya reli (hashtag) inaonekana kutekeleza ombi la Bw. Snowden kimya kimya.