Sote tunafahamu jinsi gani bidhaa za Tecno zilivyotapakaa nchi za Afrika kwa kutokea kupendwa na wengi, sababu kubwa ikiwa ni unafuu wa kuweza kupata simu husika.
Kwenye ushindani kati ya pande mbili au zaidi lazima atokee mmojawapo ambae ni bora zaidi kuliko wengine na ndivyo ilivyotokea kwa Tecno baada ya kushinda “Simu bora ya mwaka 2018” kupitia Tecno Phontom 8 tuzo zilizoandaliwa na Mobex Innovation Africa.
Tecno Phantom 8 ilishindanishwa na rununu Huawei Y7, Tecno Camon X na Nassco katika hafla iliyofanyika Septemba 29 2018 huko Ghana.