Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), limetoa gawio la Tsh. 1.5 bilioni kwa serikali, fedha zilizotokana na faida ya Tsh. 28.5 bilioni ya shirika hilo kwa mwaka jana. Shirika hilo lilipata faida ya Tsh. 29.2 bilioni kabla ya kukatwa kodi.
Akizungumza leo mbele ya rais John Magufuli wakati wa hafla ya kupokea gawio hilo, Afisa Mkuu Mtendaji wa TTCL, Waziri Kindamba amesema faida hiyo inatokana na mabadiliko makubwa yaliyoanza kuonekana kupitia uongozi wa awamu ya tano.
Pia, katika juhudi za kuimarisha shirika hilo, wameanza kutekeleza maagizo ya serikali kwa kutoa gawio hilo la bilioni 1.5 baada ya kupunguza safari za nje kwa watendaji wake na kufuta mikataba mibovu isiyokuwa na manufaa kwa shirika hilo.