Nyaakti za asubuhi, mchana mpaka jioni kasi ya intaneti kwa mitandao mingi ya simu huwa si nzuri lakini kwa usiku kasi yake (intaneti) inaongezeka mara dufu hasa kulingana na eneo husika.
Usiku wakati wengine wamepumzika kwa baadhi ya watu ndio muda mzuri wa kufanya kazi kwa njia ya mtandao, kusoma, kufanya mitihani au hata kumalizia kazi kabla hakujapambazuka. Na katika dunia ya leo intaneti inachukua nafasi kubwa sana katika kufanikisha masuala mbalimbali pamoja na niliyoyaainisha.
Kwa maoni yangu naamini kutokana na idadi kubwa ya watu kutumia sana intaneti nyakati asubuhi mpaka jioni ndipo wazo la vifurushi ya usiku lilipozaliwa ili kuwawezesha wale ambao walishindwa kutumia kifurushi vizuri mchana basi watumie usiku pamoja na intaneti yenye kasi zaidi.
Vifurushi ya namna hii (vile vya usiku) vimelenga zaidi wale ambao wanapenda intaneti yenye kasi zaidi vilevile isisyokwamakwama kutokana na kile kitu ambacho mtu anataka kukikamilisha kwa usiku huo.
Kwa yeyote anayependa kutumia intaneti nyakati za usiku mpaka alfajiri, Tsh. 500 kwa 2GB au Tsh. 1,000 kwa GB 10 kwa intaneti ya TTCL siwezi kusema kuwa mtu atakuwa ametumia pesa yake vibaya.
Chanzo: Tovuti-TTCL
One Comment
Comments are closed.