iPhone XS Max inayomilikiwa na Nyota anayetajwa wa muda wote katika historia ya mpira wa miguu, leo simu ya Messi imekuwa ndio simu yenye kava ghali zaidi Duniani kwa toleo hilo la iPhone.
Simu hiyo ya Messi imeongezeka thamani yake ya kawaida baada ya simu ya mchezaji huyo kufunikwa kwa Dhahabu halisi yenye thamani ya juu zaidi, kazi iliyofanywa na iDesign Gold.
Uboreshwaji wa simu hiyo na kampuni ya iDesign Gold kwamba dhahabu iliyotumika kubadili muonekano wake wa awali unakadiriwa kugharimu kiasi cha Dola za kimarekani 21,000 ambayo takribani Shilingi ya kitanzania 50 milioni.
Nyota mwenzake wa FC Barcelona, Ivan Rakitic pia alitengenezewa kava la dhahabu na kampuni hiyo.
iDesign Gold imetoa iPhone zilizoboreshwa kwa nyota kadhaa za soka katika miezi michache iliyopita, ikiwa ni pamoja na Dele Alli (Tottenham Hotspur), Arturo Vidal (FC Barcelona), na hata nyota wa zamani wa Liverpool Steven Gerrard.
Dhahabu hiyo ya kiwango cha Carat 24, imepamba upande wote wa nyuma ya simu hiyo kwa kuweka namba 10 inayovaliwa na mchezaji huyo, pamoja na majina ya watoto wake na la mke wake.
Simu ya iPhone XS Max (iPhone ‘Ten S’ Max) ilizinduliwa mwaka 2018 mwezi Septemba sambamba na iPhone XS na iPhone XR.
Je, una mtazamo gani juu ya kava hili la simu?
Shukrani: Akaunti ya instagram ya fcbarcatz unaoandika habari za klabu ya FC Barcelona na wachezaji wake kwa lugha ya kiswahili na mitandao mbalimbali