Hakika, teknolojia ya simu imesaidia sana hata hivyo bado imefanya vifaa vingine kufa au kupoteza muonekano wake katika macho yeto. iPod Touch ni moja kati ya bidhaa kutoka Apple ambazo ziliwahi kufanya vizuri sana.
Siku hizi nyimbo na video zote unatazama na kusikiliza kwenye simu. Pia ikumbukwe kuwa Apple walikua kama wamekisusa hiki kitengo kinachoshughulika na iPod Touch maana kwa muda kimekua hakiongelewi wala hatuoni matoleo mapya.
Sasa basi, maswali yamekua ni mengi sana kwa baadhi ya watu wanaosubiri ujio wa bidhaa kwa hamu. Fununu zinasema kuwa kuna vitu vya muhimu kama vile prosesa ambacho kwa hali kubwa kinadhaniwa kitabadilika.
Lakini katika ujio mpya wa iPod Touch si vibaya kuweza kufikiria kuwa inaweza ikaja na ile teknolojia ya Face ID iliyopo katika vifaa vyake vingine.
Kinachofurahisha kutoka kampuni hii ni kwamba bado haijaisahau bidhaa hii na bado inajua kuna baadhi ya watu wanahitaji bidhaa kama hizi katika soko, ndio maana imekataa kabisa kuachana na hii bidhaa…. pengine labda baadae!