Baada ya miezi kadhaa ya kazi, hatimae waendeshaji wa programu ya Skype wamefanikisha mawasiliano yote ya watumiaji wake kuwa ni siri.
Skype kama programu zingine kadhaa nao wameanza rasmi kutumia mfumo wa end-to-end encryption ambapo maana yake ni kwamba mawasiliano baina ya watu wawili au zaidi yanabaki kuwa salama na kuonekana kati yao tuu na si kwa wahusika wa programu au mtu mwingine wa ziada.
Pia watumiaji wa Skype wataweza kuficha mawasiliano yao yote kwa mtu mwingine kuyaona hata pale watakapoacha kufuta ujumbe au mazungumzo kwa njia ya sauti katika vifaa vyao.
Hatua hii ya kutumia mfumo wa usiri itawafurahisha watumiaji wengi ambao kwa muda mrefu walikuwa na wasiwasi wa usalama wa mawasiliano yao wanayoyafanya kupitia programu hiyo ya Skype.
Skype imekuwa programu inayopatikana katika mifumo endeshi takribani yote muhimu kuanzia kwenye simu za Android, iOS pamoja na kompyuta kwa mfumo wa Windows.