Samsung Fold zaharibika baada ya utumiaji wa muda mfupi kwa waandishi wa habari kadhaa waliopata nafasi ya kujaribu toleo hili jipya la simu inayokunjika display kutoka Samsung.
Simu ya Samsung Fold ni moja ya simu mpya za kwanza kuja na uwezo wa display/vioo vya mkunjo – yaani unaweza kuifunga na kufungua ili kuweza kupata nafasi kubwa zaidi ya display. Unaweza kusoma uchambuzi wetu kwa undani hapa -> Uchambuzi wa Samsung Fold
Imetokeaje?
Samsung wametuma simu hiyo mpya kwa waandishi mbalimbali katika vyombo vya habari vikubwa Marekani na barani Ulaya kwa ajili ya uchambuzi.
Waandishi wa habari kadhaa wameripoti display ya simu hiyo kuharibika na kutoweza kutumika tena baada ya utumiaji wa muda mfupi.
Kisa kikuu inaonekana kuna waliotoa kitu kilichoonekana kama vile ni ‘screen protector’, kumbe kilikuwa ni aina nyingine ya display ambayo ni muhimu katika ufanyaji kazi wa simu hiyo. Kutolewa kwa kipande hichi cha display kinachounganisha upande wa kulia na kushoto wa display kuu una madhara makubwa kwa ufanyaji kazi wa display ya Samsung Fold.
Ni kwa waandishi wa habari wachache ndio simu hiyo ilisumbua display bila wao kuondoa display hii spesheli. Kwa vyovyote vile Samsung itawabidi walifanyie kazi jambo hili, ingawa tayari nyuma ya simu hii onyo dhidi ya kuondoa display spesheli ya juu ilishawekwa bado inaonekana kuna mambo ya kuboresha kabla watu kutoa zaidi ya Tsh milioni 4 kwa ajili ya kununua simu hii.
Vipi nini mtazamo wako juu ya simu hii na bei yake? Soma uchambuzi kwa undani – Samsung Fold.
Vyanzo: BBC na vinginevyo