India imekuwa nchi ya kwanza duniani kutuma angani sateliti nyepesi zaidi kupata kutokea.
Kwa mujibu wa habari zilizotolewa na vyombo vya habari kadhaa kundi moja la wanafunzi wenye vipaji wa elimu ya anga walitengeneza satelaiti hiyo waliyoiita Kalamsat-V2, na ilirushwa angani na shirika la utafiti wa mambo ya anga la India (ISRO) katika kituo cha anga Sriharikota.
Satelaiti hiyo (Kalamsat-V2) imeyoundwa/kujengwa na wanafunzi wanaofanya kazi na shirika binafsi liinaitwa “Space Kidz India” huko Chennai, India.