Baada ya kuandikwa sana kuhusu taarifa za Samsung kuja na simu yake ya mkunjo, hatimae kionjo cha namna simu hiyo itakavyokuwa na muonekano wake umeonyeshwa rasmi.
Kidokezo hicho cha muonekano wa simu janja ya mkunjo kutoka Samsung umeonyeshwa kwenye mkutano wa mwaka wa wakuzaji wa bidhaa za Samsung 2018 (SDC 2018) uliofanyika huko San Francisco, Marekani.
Hii ni ahadi iliyotolewa mwezi uliopita katika jiji la Kuala Lumpur wakati wa uzinduzi wa Galaxy A9, na DJ Koh, rais na Kkiongozi Mkuu Mtendaji wa Samsung kitengo cha simu za mkononi.
Simu hiyo ya Mmkunjo itakuwa na muunganiko wa bidhaa mbili kwa pamoja ambazo ni tabiti na simu janja. Ikikunjuliwa itakuwa na muonekano wa tabiti na ikikunjwa itakuwa na muonekano wa simu janja.