Kampuni ya simu za Samsung imeendelea kuongoza katika soko la kimataifa la simu duniani mpaka kufikia mwezi Aprili huku simu zinazozalishwa Uchina zikipata nafasi za juu katika soko kwa mwaka 2018.
Kwa mujibu wa kampuni ya utafiti ya StatCounter simu za Samsung zimepanda kwa asilimia 0.1; Februari 2018 Samsung waliuza simu zao kwa asilimia 31.9 ukilinganisha na Februari 2017 ambapo waliuza asilimia 31.8 kwa simu zote zilizouzwa katika masoko ya dunia.
Apple imeendelea kuwa nafasi ya pili kwa kuchangia soko la simu janja kwa kuuza kwa asilimia 20.1 kwa mwezi Februari. Mwezi Januari 2018, Apple waliuza kwa asilimia 19.6 na iujumla mauzo ya bidhaa za Apple mauzo yake yamepanda kwa asilimia 0.5.
Washindani wengine.
Huawei imeshika nafasi ya tatu duniani kwa mauzo ya simu janja kwa soko la kimataifa baada ya mauzo yake kupanda kwa asilimia 0.2. Mwezi Februari 2018 waliuza kwa asilimia 5.5, dhidi ya 5.3% ya Januari 2018.
Ripoti pia imeonesha ukuaji wa soko la kimataifa kwa simu za Xiaomi kwa mwezi Februari, kwa kushika nafasi ya nne nyuma ya Huawei. Soko la Xiaomi liliongezeka hadi 5.1% mwezi Februari 2018 kutoka asilimia 4.8 mwezi Januari 2018.
Oppo ya Uchina imeshika nafasi ya tano kwa upande wa soko la dunia la simu janja, kwa kuuza 3.6% mwezi Februari 2018, kutoka asilimia 3.4 mwezi Januari 2018.
Wakati huohuo, LG imeuza 3.4% kwa mwezi Februari 2018, wakati mauzo ya bidhaa za Lenovo yameshuka kutoka 2.8% Januari 2018 hadi 2.7% mwezi Februari 2018, lakini bado imeendelea kushika nafasi ya saba kwa mwezi wa pili mfululizo katika soko la kimataifa la simu janja.
Motorola nayo imeuza kwa 2.5% mwezi Februari 2018, ikiwa imeshuka kutoka mauzo ya asilimia 2.6 kwa mwezi Januari 2018.
Nokia imekuwa ya mwisho kati ya wazalishaji wa juu katika soko la kimataifa kwa kushuka mauzo yake ya Februari 2018 kulinganisha na ya Januari 2018. Mwezi Februari waliuza kwa asilimia 1.7 wakati Mwezi Januari iliuza kwa asilimia 2 na sehemu yake ya soko kiujumla kufikia asilimia 1.7.