Samsung Galaxy yenye 5G ni moja ya simu ambazo zimekuwa zikiongelewa kuhusu ujio wake tangu mwaka uliopita na kwenye onyesho la bidhaa la kielektroniki (CES) mwaka 2019 hilo lilidhihirika.
Mengi yalionekana kwenye onyesho la bidhaa za kielektroniki ambalo hufanyika kila mwaka Samsung wao waliweka kielelezo cha simu yao ambayo inaaminika kuwa ya 5G kutolana na kuwa kwenye mstari ambao rununu za teknolojia hiyo (5G) zionekane.
Wakati simu hiyo ilipokuwa imewekwa kwenye onyesho hilo aarifa zinadai kuwa haikuwa imeunganishwa na teknolojia ya 5G. Watu wanasubiri kuona iwapo simu hiyo itakuwa ni miongoni mwa zile zitakazozinduliwa Feb 20 2019.
Vyanzo: GSMArena