Kwa wale wapenzi wa simu za Android na wale ambao wanafikiria kununua simu mpya na mshiko upo wa ukweli nawashauri mjipe ‘stop’, mvute pumzi kidogo na kusubiria a.k.a kutafuta kitu moto toka Samsung, nacho ni Samsung Galaxy III.
Hakuna siri ya kuwa simu za Android ni nzuri sana, kwa wale wapendao simu wanayoweza kuifanyia maujanja na kuongeza ma’tweaks’ na wakadhalika na matumizi ya picha, video na matumizi ya intaneti si utani Android zipo poa.
Sasa turudi kwenye Samsung Galaxy S ya 3. Simu hii imeingia sokoni hivi karibuni, tayari ishapigiwa ‘pre-orders'(yaani washalipa kabla ya kukitia mkononi/machoni ‘live’) ya zaidi ya watu milioni 7 (PC Adviser), na kuvunja pre-orders za simu nyingine nyingi kutoka kwa wapinzani.
Hii si mchezo, na ipo katika uwezekano mkubwa kuwa simu itayouzika kwa wingi zaidi ndani ya muda flani katika simu za Android.
TANGAZO LA SAMSUNG GALAXY SIII
Inauwezo wa kuzima/kupunguza mwanga wa kioo (screen)
pale utakapoacha kuitazama au kusinzia..upo?
Kama umeiweka kona na unataka kujifotoa usiwe na hofu chagua
kwa kamera, weka pozi afu sema ‘cheese’
nayo itajipiga!
Au unamuandikia mtu meseji afu ukaona isiwe tabu ngoja umpigie,
cha kufanya ni wewe kupeleka simu kwa sikio nayo itampigia yenyewe!
Unene: Inchi 3.4
Ukubwa wa ‘screen’: Inchi 4.8
RAM: 2GB
Android 4.0 ICS
Na Nafasi ya kuweka Mafaili ya ukubwa wa 16GB na 32GB
TUNAKARIBISHA MADUKA/DEALERS WENYE BIDHAA MPYA
KAMA SIMU, KAMERAS, LAPTOPS, DESKTOPS,TABLETS N.K
KWA REVIEWS NA KUJITANGAZA, KUA NASI!
No Comment! Be the first one.