Tovuti mbalimbali zimekuwa zikifuatilia habari kuhusu ujio wa Samsung Galaxy S10 ambapo mpaka sasa yapo mambo kadha wa kadha yameshafamika ila zote zikiwa ni fununu tu lakini ukweli wenyewe utafahamika Feb 20 2019.
Kwa wiki kadhaa imekuwa ni ngumu kuperuzi tovuti mbalimbali na ukose kukutana na habari inayozungumzia kuhusu sifa ambazo rununu husika itakuwa nazo na hata sisi wenyewe, TeknoKona tumeshaleta habari hizo>>>KUHUSU SAMSUNG GALAXY S10.
Wakati wa kupata fununu sasa unafikia ukingoni baada ya kutoka tangazo rasmi kuhusiana na uzinduzi wa simu janja, Samsung Galaxy S10 ambazo zinategemewa kutoka toleo zaidi ya moja.
katika uzinduzi huo inategemewa kuona simu janja Samsung Galaxy S10, S10+ na S10 E. Unatakiwa ukae kusubiri kwani tutaziangazia simu husika mara tu zitakapotoka.
Vyanzo: GSMArena, CNET