Imepita miezi miwili sasa tangu kampuni pendwa ya simu za mkononi ya Samsung kuitambulisha simu yao yenye muonekano tofauti kabisa katika soko la simu. Sasa imeshafahamika ni lini simu hiyo itaingia sokoni.
Rununu, Samsung Galaxy F ni simu inayojikunja imekuwa ikiongolewa na watu wengi sana na imekuwa chini ya kampuni yao tu kwa muda wote na kutoruhusu mtu yeyote kuigusa. Kuanzia jana tarehe 15/04/2019 wahusika waliweza kuruhusu watu mbali na wachambuzi wa simu kuzigusa na kupiga picha.
Simu hii itaanza kupatikana na kuuzwa rasmi kuanzia tarehe 26 mwezi huu wa nne. hivyo kama wewe ni mpenzi mzuri wa simu mpya za kisasa basi kuanzia tarehe iyo unaweza pitia katika stoo zao za SAMSUNG.