Kampuni ya mawasiliano, Safaricom imeendelea kutamba baada ya kupata ongezeko la faida asilimia 20.22 kwa miezi sita kufikia Septemba 2018. Ongezeko hilo linahusishwa miamala ya M-Pesa kufanyika mara dufu.
Ripoti hii ni kulingana na kampuni hiyo ni baada ya kutozwa kodi, Safaricom iliripoti faida ya Ksh. 31.5 bilioni ikilinganishwa na Ksh. 26.20 bilioni mwa mmoja uliopita.
Kampuni hiyo ya mawasiliano ambayo hisa zake katika soko la hisa la Nairobi zilizaa Ksh. 35.52bn kutoka M-Pesa, ongezeko la asilimia 18 kutoka Ksh. 30.05 bilioni mwaka mmoja uliopita.
Ukuaji wa matumizi ya intaneti yalipungua katika kipindi hicho, ambapo watumiaji katika kipindi hicho waliipa kampuni hiyo Ksh. 19.45 bilioni. Mapato kutokana na kupiga simu yaliongezeka asilimia 1.4, hadi Ksh. 48.03 bilioni.
Mapato yote ya Safaricom ambayo yanajumuisha vitu vingine ambavyo kampuni hiyo inauza mathalani rununu pamoja na vitu vingine yamefikia Ksh. 122.84bn kutoka Ksh. 114.43bn mwaka jana.
Ulikuwepo mpango wa kufanya M-Pesa na Safaricom kuwa kampuni mbili tofauti lakini suala hilo likawekwa kando mwezi Januari mwaka huu.