Simu janja nyingi zimekuwa zikikabiliwa na tatizo la kutokaa na umeme kwa muda mrefu kitu ambacho kinasababisha mtu kufikiriakubadilisha betri kitu ni gharama lakini si pale ambapo kuna punguzo la bei.
Mwezi Desemba ni mzuri kwa yeyote yule ambae antumia iPhone kwani kampuni husika imetangaza punguzo la bei kwa betri ya iPhone SE mpaka iPhone X.
Ofa hiyo itadumu mpaka Desemba 31 ambapo bei ya betri itakuwa ni $29|Tsh. 66,700 kutoka $79 ambayo ni sawa na Tsh. 181,700.
Mwaka 2019 ukitaka kufanya matengenezo ya iPhone toleo la zamani kidogo itagharimu $49|Tsh. 112,700 lakini betri ya iPhone X itabadilisha kwa $69|Tsh. 158,700.
Vyanzo: Forbes, GSMArena