Sio simu zote za Samsung zimepata au zitapata masasisho ya programu endeshi toleo la nane maarufu kama Oreo lakini kwa wanaotumia Samsung Galaxy J7 Prime watafurahi kwani sasa wanaweza kuhamia kwenye Android 8.
Katika mpango wa Samsung kupeleka masasisho ya programu endeshi ilibainisha simu ambazo zilitoka mwaka 2016 zilizo na progragramu endeshi-Marshmallow zitapokea masasisho na kuweza kuhamia toleo la Oreo.
Kabla hujafikiria kuhamia kuhamia kutoka toleo moja hadi jingine ni muhimu sana kuhakikisha simu/kifaa husika kina chaji angalau 50% na kuendelea, mpangilio wa intaneti uko sawa lakini kubwa zaidi kuwa na kifurushi cha intaneti zaidi ya 1024MB (1GB).
Masashisho ya Oreo kwenye Samsung Galaxy J7 Prime utegemee kuona maboresho kwenye muonekano wa vitu kwenye uso wa mbele, kipengele cha Smart View, Samsung Cloud, n.k. Kushusha/kuhamia kwenye Android 8 kitu chote kina ukubwa wa 1040MB (zaidi ya GB 1).