Katika moja ya makampuni ambayo yanaleta ushindani dhidi ya wakongwe ni Oppo ambapo kiujumla bidhaa zao zimekuwa zikikubalika na kuifanya kampuni husika kuwa kwenye nafasi za juu kiushindani na siku si nyingi zilizopitawametoa Oppo A5s.
Oppo imekuwa ni zile kampuni ambazo zinayoa simu janja mara kwa mara; inawezaikawa ni muendelezo wa toleo fulani au ikawa ni rununu ambayo ni kutoka familia mpya kabisa. Kwa Oppo A5s ni muendelezo tu wa iliyomtangulia (Oppo A5) na kimsingi tofauti kati ya simu hizo ni kwenye baadhi ya vipuri.Simu hii ambayo naiangazia leo kwa jina lingine inafahamika kama “AX5s” na sifa zake ni kama ifuatavyo:-
Kipengele |
Maelezo |
Kipuri mama+Ufanisi | Mediatek MT6765 Helio P35, vipuri nane (8) vyenye kasi ya 4×2.3 GHz Cortex-A53 na 4×1.8 GHz Cortex-A53,
Kipuri kinachofanya ung’avu wa picha ni PowerVR GE8320 |
Kioo+muonekano | Kina chake ni aina ya IPS urefu wa inchi 6.2 (720 x 1,520px). Kwenye uso wa mbele ina duara dogo lililoizunguka kamera ya mbele |
Kamera | Kamera ya nyuma: MP 13+MP 2
Kamera ya nyuma: MP 8 |
Kipengele |
Maelezo |
RAM+Diski uhifadhi |
Ina GB 3 za RAM, GB 64 memori ya ndani lakini pia inawezekana kuongeza memori ya ziada mpaka GB 256 |
Betri+Programu endeshi |
Betri yake hatoki na ina 4320mAh, imewekwa Android 8.1 Oreo kama programu endeshaji |
Rangi+Mengineyo |
Ipo katika rangi Nyekundu na Nyeusi. Inatumia teknolojia ya alama ya kidole, ina sehemu ya kuchomeka spika za masikioni, redio, Bluetooth, Wi-Fi, inatumia USB OTG |