Kwa miaka kadhaa BlackBerry katika matoleo ya simu zake imetumia kicharazio (Keyboard) halisi kuwashawishi watumiaji wake kwamba ni kicharazio kizuri na kisicho kufa kirahisi.
Kwa sasa simu zinazotumia jina la Nokia zinatengenezwa na kampuni inayokwenda kwa jina la HMD.
Hata hivyo takwimu zinaonesha keyboard hizo hazipendwi tena na watumiaji wengi zaidi ya zile za kisasa za mguso (touch). Pamoja na hali hiyo Nokia wameamua kuja na simu yenye keyboard halisi. Simu janja hiyo ambayo bado haijajulikana itakuwa na jina gani lakini model yake ni TA-1047.
Simu janja hiyo tayari imepata kibali cha kuidhinishwa na kuthibitishwa na tume ya ushindani Fair Competition Commission (FCC). Simu hiyo inaonekana itakuwa ndogo yenye keyboard halisi kama ya simu za nyuma za Blackberry.
Kama taarifa ni za kweli kuhusu sifa za simu hiyo basi itakuwa na kioo kidogo chenye 3.3inchi na 480×480 display resolution. Itakuwa na prosesa ya Qualcomm Snapdragon 230 na itakuwa na mfumo endeshi wa KaiOS. Haijajulikana kama itauzwa kwa masoko yote dunia na gharama yake itakuaje ingawa inaonekana itakuwa simu ya gharama nafuu.
Taarifa za ujio wa simu hiyo kumezua mijadala mingi kwa watu wenye kufatilia ulimwengu wa teknolojia ya simu. Ni kwamba Nokia wanarudi katika ubora wao wa zamani katika simu au ndio wanapotea.