Mwanamke ambaye anataka kutumia mayai ya uzazi ya bintinye ili kumzaa mjukuu wake ameshinda kesi mahakamani na kuruhusiwa kufanya hivyo.
Mwanamke huyo wa umri wa miaka 60 alikuwa amekatazwa kupeleka mayai ya bintiye kwenye kliniki moja nchini Marekani hali iliyosababisha akate rufaa. Bintiye ambaye aliaga dunia mwaka 2011, anaripotiwa kumuambia mamake amzalie watoto wake lakini mamake alishindwa katika kesi mwaka uliopita.
Hata hivyo aliruhusiwa kupinga hukumu hiyo katika mahakama ya rufaa. Mwaka 2014 halmashauri inayohusika na mayai ya uzazi, ilisema kuwa mayai hayo yasingeruhusiwa kutoka mjini London kwa sababu bintiye hakuwa ametoa idhini kamili kabla ya kifo chake.
Lakini kwenye kesi ya sasa mawakili waliwaambia majaji kuwa, mwanamke huyo alikuwa anataka kutimiza matakwa ya bintiye ya kuzaa mtoto akitumia mayai yake na kisha amlee mtoto huyo.
Kwa sheria za Uingereza hakuna ukomo wa umri kumzuia mwanamke kupandikizwa mayai ambayo yalikuwa yametunzwa na hatimaye kuweza kuzaa baada ya miezi ya kujifungua kutimia.
Nia ya mwana mama huyo kuyapeleka mayai hayo New York Marekani ni kwenda kutafuta mbegu ya kurubisha mayai hayo na kisha kupandikizwa kuweza kubeba na kulea mimba hiyo.
Je, unadhani mwanamke huyo atashinda rufani yake kutokana na maelezo yake? Endelea kufuatilia Teknokona nasi tutazidi kuwataarifu.
Makala hii imeandikwa kwa usaidizi wa vyanzo mbalimbali: BBC, The Telegraph na Women’s health.