Mamlaka za usalama nchini Uganda kwa kushirikiana na idara ya uhamiaji imemfukuza mkurugenzi mtendaji wa kampuni kubwa ya mawasiliano ya simu nchini humo ya MTN, Wim Vanhelleputte kutokana na sababu za kiusalama.
Kampuni hiyo ya MTN imeandika katika ukurasa wake wa Twitter kuwa haijafahamishwa sababu za kufukuzwa kwa mkurugenzi huyo, hata hivyo, msemaji wa jeshi la polisi nchini Uganda Fred Enanga amesema, Vanhellepute, raia wa Ubelgiji, amefukuzwa kutokana na tuhuma za kutishia usalama wa taifa.
Mkurugenzi huyo ni mwajiriwa wa nne wa kampuni hiyo ya Afrika Kusini kufukuzwa katika wiki chache zilizopita, akifuatia kufukuzwa kwa waajiriwa raia wa Ufaransa, Rwanda, na Italia.
Barua iliysainiwa na waziri wa mambo ya ndani wa nchi hiyo Jeje Odongo imeonyesha kwamba Wim Vanhelleputte hakubaliliki tena kuwepo nchini Uganda na akae mbali kabisa na nchi hio milele.
Taarifa zisizorasmi zinasema wafanyakazi hao wa MTN wamekuwa wakihusika na kutuma taarifa nyeti za viongozi wa nchi kwa vyombo vingine vya kijasusi – hasa hasa vile vya Rwanda. Tayari mataifa ya raia hao yametaka ripoti ya uhakika kutoka Uganda juu ya tuhuma hizo.
Taarıfa kutoka polısi zinasema Mkurugenzi huyo alisafirishwa siku ya Alhamisi.