Moja ya simu ambazo zilitokea kununuliwa sana kipindi hicho ni Motorola RAZR ambapo ndio ilikuwa kwenye umaarufu wake.
Unaweza usiikumbuke kwa jina lakini ukiona picha utaikumbuka vyema hasa kwa wale waliokuwa wanatumia kipindi hicho kuona fahari kuwa na rununu ya kuvutia kweli.
Motorola wanaonekana kufuata nyayo za Nokia ambao pia walitoa simu zao za toleo la zamani lakini katika muonekano mpya pamoja na maboresho mengineyo; hapa nazungumzia NOKIA 3310 na NOKIA 8110.
Motorola ambayo kampuni mama ni LENOVO wanatazamiwa kuzalisha takribani simu laki mbili kwa idadi ya toleo hilo jipya.
Kuhusu toleo jipya la Motorola RAZAR hakuna kunachofahamika zaidi ya kujua kuwa itakuwa ni ya kukunja na kukunjua, itatoka mapema mwezi Februari 2019 na bei yake itakuwa ni $1,500|zaidi ya Tsh. 3,4450,000.
Vyanzo: Wall Street Journal, The Verge
2 Comments
Comments are closed.