Jarida la Forbes, limetoa orodha ya matajiri wa kupindukia duniani na kumtaja mmiliki wa Kampuni ya Amazon, Jeffrey Preston Bezos kuwa kinara katika orodha hiyo.
Utajiri wa Bezos umepanda na kufikia dola bilioni 112 kutoka takriban dola bilioni 39.2 za mwaka jana. Jeffrey Bezos ndiye mmiliki na mwanzilishi wa Mtandao maarufu duniani wa uuzaji na ununuzi bidhaa mbalimbali.
- Kuimarika kwa utajiri wa Bezos katika historia, kumemuondoa mwanzilishi wa Microsoft Bill Gates kutoka katika orodha hiyo kama tajiri namba moja.
- Katika orodha hiyo mpya, tajiri Gates mwenye utajiri unaokadiriwa kuwa wa dola bilioni 90 mwaka huu kutoka bilioni 86 ndiye anayeshikilia nafasi ya pili.
Gates ameongoza orodha hiyo kwa miaka 18 kati ya miaka 24 iliyopita.
Miongoni mwao, kuna mabilionea 259 wapya ambao walijipatia utajiri wao kutoka katika biashara za aina nyingi zikiwemo nguo za harusi, wanasesere wa kuchezewa na watoto na magari yanayotumia umeme.