Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Fedha la mradi wa Cradle Fund la Malaysia, Nazrin Hassan ameripotiwa kufa kutokana na majeraha aliyoyapata yaliyosababishwa na mlipuko wa simu ya mkononi.
Awali ilielezwa sababu ya kifo chake ni tatizo la kupumua lakini kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Cradle, Nazrin Hassan alikufa kwa matatizo ya majeraha aliyoyapata kichwani kutokana na mlipuko wa simu wakati alipokuwa amelala.
Haijajulikana ni simu aina gani iliyolipuka na kusababisha kifo chake. Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari vya Malaysia kutoka kwa familia ya Hasssan zinaeleza alikuwa na simu mbili moja BlackBerry na nyingine Huawei, lakini haijafamika ni ipi iliyolipuka.