Timu ya madaktari wamefanikiwa kufanya upasuaji na kuutoa mkasi ndani ya tumbo la mwanaume mmoja huko Vietinamu, mkasi huo ambao ulisahauliwa katika upasuaji mwingine aliofanyiwa mgonjwa huyo miaka 18 iliyopita.
Ma Van Nhat mwanaume wa miaka 54 alikuwa amekwenda hospitali kwaajiri ya matibabu baada ya kupata ajali ya barabarani, katika matibabu hayo ndipo mkasi huo ulipogundulika ndani yake.
mkasi huo ambao unatumiwa na madaktari nyakati za upasuaji ulikuwa na urefu wa sentimita kumi na tano, ulikutwa ukiwa na kutu na tayari umekwisha katika katika vipande viwili.
Jamaa huyo alipohojiwa anasema baada ya upasuaji wa mwaka 1998 alirudi nyumbani lakini aliendelea kusikia maumivu hali iliyopelekea kwenda tena hospitali hata hivyo huko aliambiwa kwamba anavidonda vya tumbo jambo ambalo lilipelekea kuendelea kutumia dawa za kutuliza maumivu.
Mgonjwa huyo alifanikiwa kufanyiwa upasuaji salama siku ya tarehe 31 mwezi wa kumi na mbili mwaka jana na mkasi huo kuondolewa, hospitali alipofanyiwa upasuaji huu kuondoa mkasi huu ndiyo hospitali ulipofanyika upasuaji uliosahau mkasi ndani yake miaka 18 iliyopita.
Hospitalli hiyo imekili kosa hilo lakini ikasema ni ngumu kujua ni nani hasa walihusika katika upasuaji huo wa kwanza kwa kuwa hawatunzi rekodi zaidi ya miaka 15 na kuongeza kwamba watajitahidi kutafuta ni nani walifanya kosa hilo na kisha kuwajulisha.