Microsoft wazuia sasisho (updates) kwenye baadhi ya kompyuta zinazotumia Windows 10. Sasisho linalozuiwa na Microsoft inasemekana linaweza sababisha matatizo makubwa kwenye kompyuta ambazo zimezuiliwa kuingia.
Kutokana na uamuzi wa Microsoft sasisho la mwezi Mei (May 2019) ambalo tayari limeanza kupatikana halitakubali kwenye kompyuta zote kudownload.
Tatizo gani:
- Kimakosa, sasisho hili linaweza fanya programu endeshaji ya Windows ijichangaye kwenye rekodi za diski au vifaa vya USB vilivyochomekwa kwenye kompyuta husika. Mchanganyo wa rekodi hii inaweza sababisha Windows isiwake/kutambulika au ata data za Diski zingine kuharibika kimakosa.
Masasisho ya Windows 10 yamekuwa mara nyingi yanakuja na matatizo mbalimbali na hili la sasa inaonekana Microsoft wametambua mapema na kuona njia pekee ni kuzuia kompyuta kupokea sasisho hili.
Ukienda sehemu ya kupata masasisha Windows itakupa taarifa kuhusu jambo hili, ila kama kompyuta yako inatumia diski moja tuu (Disk C) basi cha kufanya ni kuhakikisha umechomoa vifaa vingine vyote vya USB wakati unasasisha kompyuta yako.