Kuna uwezekano mkubwa Microsoft kuondoa programu ya Paint katika sasisho (update) jipya la Windows 10.
Programu ya Paint inayomuwezesha mtumiaji kuweza kutengeneza michoro mbalimbali kwa urahisi na bila ujuzi mkubwa sana wa kisanii imekuwa katika matoleo ya programu endeshaji ya Windows tokea Novemba mwaka 1985 kwenye toleo la Windows 1.0.
Programu ya Paint imekuwa ni rahisi kwa watumiaji wengi katika suala la ubunifu wa picha ukilinganisha na programu zingine zinazoitaji ujuzi zaidi kama vile Adobe Photoshop.
Imekuwa ikipata maboresho mapya mara kwa mara na wakati wote imeendelea kuwa programu ya bure. Katika sasisho (update) jipya linalokuja lililopewa jina la Windows 10 Fall Creators Update programu hiyo imewekwa kwenye kundi la vitu vinavyouliwa.
Tayari Microsoft wameshaleta programu mpya ambayo ni maboresho zaidi ukilinganisha na hii ya Paint, wameipa jina la Paint 3D na inapatikana kwenye soko la apps katika Windows 10.
Wengi wanaamini kuna uwezekano mkubwa katika sasisho hilo Paint 3D ikachakua nafasi ya programu ya Paint.