Shirikisho la wakala wa mtandao nchini Ujerumani limepiga marufuku uuzaji wa saa janja za ‘kitoto’ kwa watoto kwa madai saa hizo zinatumika kama vifaa vya upelelezi.
Marufuku hayo yatawahusu watoto wa kuanzia umri wa miaka 5 mpaka 12. Saa janja hizo zimekuwa zikionekana kama wanasesere za kuchezea lakini zimesaidia wazazi wa watoto hao kusikiliza mazungumzo yote yanayoendelea darasani baina ya waalimu na wanafunzi.
Shirikisho hilo limesema saa hizo zinakiuka sheria ya nchi ya kurekodi mazungumzo binafsi ya watu wengine bila ya ridhaa yao. Mwanasesere wa saa janja hizo anaitwa My Friend Cayla na amekuwa akitumika na wazazi kwa ajili ya kufatilia nyendo za watoto wao kwa kusikiliza na kuona eneo walipo kwa njia ya Intaneti.
Saa janja hizo zimekuwa zikitumika na wazazi wengi nchini Ujerumani kuwavalisha watoto wao kama njia mojawapo ya usalama wa kuwafatilia popote walipo hususani wanapokwenda mashuleni. Kwa mujibu wa shirikisho hilo wazazi wengi wamekuwa wakitumia mtindo huo kusikiliza mazungumzo ya waalimu darasani.