Mawasiliano kwa nja ya WhatsApp ni kitu ambacho kimeshazoeleka kwenye mataifa mengi duniani kiasi hata kuwa moja ya njia kuu ya mawasiliano baina ya mtu na mtu au kundi la watu, suala la kuweza kujua ujumbe umesambazwa mara ngapi imekuwa ni kitendawili!.
WjatsApp kama moja ya programu tumishi ambayo ina watumiaji wengi zaidi duniani imekuwa ikiboreshwa mara kwa mara kwa kuweka vitu vipya kama njia ya kuvutia watumiaji wake lakini hata kurekebisha yale ambayo yanalalamikiwa. Kwa mara nyingine imebainika kuwa WhatsApp wanafanyia majaribio vipengele viwili vipya viitwavyo “Forwarding Info” na “Frequently Forwarded“.
“Forwarding Info” maana yake nini?
“Forwarding info” ama taarifa kuhusu ujumbe uliosambazwa (kwa mujibu wa tafsiri isiyo rasmi) ni kipengele ambacho kitakuwa kinaeleza ni mara ngapi ujumbe huo umesambazwa. Sasa je, kinafanyaje kazi? Utaweza kujua ujumbe husika umesambazwa mara ngapi iwapo tu utajitumia mwenyewe ujumbe au kumtumia mtu mwingine kisha utabonyeza kwenye ujumbe husika kama unataka kuunakili kisha bofya chagua kwenye alama ya “i” utapata kujua iwapo ujumbe huo umesambazwa mara moja, mbili, n.k.
“Frequently Forwarded” maana yake nini?
Kwa tafsiri ya kawaida tuu “Frequently Forwarded” ni kitu ambacho kinasambzwa mara kwa mara yaani iwapo ujumbe/picha jongefu umetumwa kwa watu zaidi ya mara nne kwenye WhatsApp basi utakuwa kwenye kundiza jumbe zilizosambazwa mara kwa mara.
WhatsApp toleo la majaribio (BETA) 2.19.80 ndio vipenge hivyo vipya vimeonekana huko. Tusubiri kuweza kuona iwapo vitapatikana kwa wote ingawa sio lazima kitu ambacho kipo katika hatua ya majaribio basi kitaruhusiwa kutumiwa na wengine.
Vyanzo: GSMArena, Gadgets 360