Samsung ni kampuni ambayo ina watumiaji wengi wa simu janja, licha ya hivyo ni kampuni ambayo inajitahidi kuja na teknolojia ya juu katika vifaa vyakokwa sasa iko na Galaxy S10.
Toleo lake la Galaxy S10 limetoka tayari na hivi sasa ni muda mzuri kwao katika kulitangaza toleo hilo. Kwa upande wao wamekuja na njia tofauti za kutangaza vifaa vyao ukilinganisha na makampuni mengine.
Huko nchini Singapore katika vituo vya mabasi ambavyo havikaukiwi na watu kwa kiasi kikubwa wameweza kuweka mabango spesheli kwa kushirikiana na kampuni ya matangazo ya JCDecaux. Mabango haya watumiaji wa Galaxy S10 wanaweza kuyatumia ili kuchaji vifaa vyao bila chaji.
Kumbuka Galaxy S10 inakuja na uwezo wa kuweza kuchaji simu hiyo bila ya kutumia kimemeshi. Vituo hivyo vinajulikana kama “Power sharing stations“.
Lakini jambo kama hili sio la kushangaza sana kutoka kwao Samsung kwani wameshawahi hata kuleta teknolojia kama hii; wiki kadhaa tuu zilizopita waliweza kutumia teknolojia hii katika mabango hayo huku wakiwa wanatangaza ni jinsi gani teknolojia ya kuchaji bila chaja kunafanya kazi.
Kwa jambo hili kampuni tunaipongeza sana maana inajitangazia biashara ya simu husika wakati na watumiaji wa simu hizo wanafaidika vilivyo na teknolojia hiyo endapo simu zao zitakua zimeishiwa na umeme lakini pia kama watakua meneo ya karibu na vituo hvyo.
Teknolojia hii inaonekana kama ina tija na watu ambao washaanza kuitumia wametokea kuipenda, kuna hati hati kubwa teknlolojia hii ikaendelea kutumia hata katika maeneo mengine duniani.