Ukuaji wa teknolojia umekuwa chachu ya kuwafungua macho watu na kuweza kujua vitu vinavyoendelea duniani kwa njia mbalimbali na neno “Kuperuzi” sio neno geni kabisa kwa yeyote ambae anpenda kupekuapekua huku na kule mtandaoni.
Hivi sasa kuna mna mbalimbali ambazo zinamuwezesha mtu kuweza kutafuta kile anachohitaji lakini intaneti, kifaa cha kidijiti vina simama kikamilifu ili kuweza kumpa majibu mhitaji. WhatsApp imekuwa ikirahisisha mawasiliano duniani kote na kila mara inaboreshwa kuweza kuvutia kitu ambacho kinasababisha kuendelea kuwavutia watu wengi. Sasa inaweza isiwe kitu cha ajabu pale mtu atakapokuwa anatumia WhatsApp kuperuzi tovuti mbalimbali.Najua uanjiuliza mambo yanakuaje hapo?
Kama ilivyo kawaida ya makampuuni mengi yanajishughulisha na masuala ya teknolojia kujaribu vitu kabla ya kuruhusu kitu hicho kupatikana kwa watumiaji wote, WhatsApp wanajaribu kipengele kipya kwewnye programu tumishi ambapo mtumiaji wa ataweza kutumia WhatsApp kama kivinjari; kwa maana ya kwamba kuweza kutembelea tovuti yoyote (kuperuzi).
Mbali na hapo WhatsApp pia wanafanyia majaribio kipengele cha kuweza kuweka picha ambayo imetumwa kwenye WhatsApp kuiweka kwenye Google lakini kubwa zaidi kuweza kuiondoa picha husika kutoka huko mara tu utakapotaka (Reverse image).
Kitu ambacho kinaweza kutowavutia watu ni kwamba hutaweza kurekodi/kupiga picha uso wa mbele kwenye kioo kwenye WhatsApp ukiwa unatumia kuperuzi kwenye wavuti yoyote ile. Vipi una mtazamo gani kuhusiana na hilo au uwezo wa kutafuta kitu mtandaoni kupitia programu tumishi husika?
Vyanzo: GSMArena, Venture Beat