Upo mpango wa chini kwa chini kuhusu kuondolewa kwa 3D Touch kwenye iPhone kutokana na sababu mbalimbali ingawa mambo bado hayajawekwa hadharani.
Uvumi wa kutokuwepo tena kwa teknolojia hiyo kwenye iPhone unapewa nguvu zaidi na zile bidhaa (simu rununu) ambazo Apple inatazaniwa kuzitangaza kwa ulimwengu mwezi Septemba 2018.
Nini hasa ambacho kinafanya 3D Touch kufikia mwisho?
Moja ya watu kutoka kitengo cha uhandisi chini ya Apple anakiri kuweka teknolojia hiyo kwenye kioo sio kitu kirahisi na kinahitaji ustadi na gharama kubwa halafu kisitumike.
Sababu nyingine ni ufahamu. Ipo wazi kabisa kuna watu wana iPhone zenye teknolojia ya 3D touch lakini hawafahamu kama simu hizo zina kitu/kipengele hicho.
3D Touch ni nini?
Kwa lugha rahisi ni teknolojia ambayo inatoa tathmini ya kiasi gani ambacho unabonyeza kwa kuweka nguvu kidogo (kukandamiza) wakati wa kufikia programu tumishi/kucheza michezo ya kwenye simu na kitu hicho kiliekwa kwenye simu za iPhone 6s na iPhone 6s Plus mwaka 2015.
Hakuna mtu anayependa kuleta kitu halafu kisipendwe au kutouzika na kama ikiwa ni kweli basi teknolojia hiyo itakuwa imefikia mwisho na kwa wewe ambae ulikuwa haufahamu kuwa iPhone 6s/6s+ ina hicho kitu leo umejua.
Vyanzo: The Verge, Apple