Makampuni makubwa nchini Uingereza yamekuwa yakilipa kodi kama kawaida lakini kodi hiyo inaonekana kuwa haitoshi kutozwa Facebook, Google, Instagram na wengineo.
Kiongozi wa upinzani kutoka chama cha wafanyakazi nchini Uingereza, Bw. Jeremy Corbyn ameshauri kuwa makampuni nguli yaongeze kodi na kutumika kulipia tozo mbalimbali ili kuwapunguzia mzigo wa kodi wananchi wa hali ya chini.
Bw. Corbyn ameshauri tozo kwa leseni mpya ambayo itakuwa ni mbadala kwa ile ya sasa akiwalenga makampuni yanayotoa huduma za intenti, mitandao ya kijamii na nyingine zote ambazo zinapata faida kubwa.
Je, kitakachopatikana kitatumika wapi?
Kwa mujibu wa kiongozi huyo kutoka chama cha wapizani kodi hiyo itatumika kulipia huduma ya wananchi kupata matangazo ya shirika la habari BBC (British Broadcasting Corporation) ambapo kwa mwaka mwananchi anapaswa kulipia $192 ili kuweza kuangalia chaneli/kurekodi kipindi kinachorushwa mubashara kinachoonyeshwa kwenye chaneli hiyo.
Bw. Jeremy Corbyn anaamini bila kuongezea kodi kuwa juu makampuni hayo itafikia kipindi sekta ya habari (mitandao ya kijamii) itakuwa haishikiki kwa kupata faida kubwa halafu wananchi wa hali ya chini wakibaki kuteseka.
Vyanzo: Reuters, The Guardian