Katika moja ya biadhaa za Samsung ambazo zinasubiriwa kwa hamu na wateja wa simu janja ni Samsung Galaxy F, herufi “F” ikimaanisha ‘Foldable‘ yaani inayojikunja.
Yapo mengi ambayo yameshafahamika kuhusu simu yenyewe na kwa mwaka 2019 Samsung Galaxy F imebainika itakuja na idadi ya kamera tatu (3) kama ilivyo Samsung Galaxy A7 (2018).
Pia, inaaminika kabisa kioo kidogo cha simu husika kitakuwa na urefu wa inchi 4.6 na pale itakapokunjuliwa urefu wa kioo husika utakuwa ni inchi 7.3.
Samsung wanatazamiwa kutoa Galaxy F kabla ya nusu ya kwanza mwaka 2019 kumalizika lakini kabla ya hapo tutegemee kuiona Samsung Galaxy S10+ ambayo pia itazamiwa kuwa na kamera tatu kwa nyuma.
Vyanzo: GSMArena, India Today