Kampuni ya Jumia imejikuta katika skendo inayohusisha udanganyifu wa data za kimapato na wateja ikiwa ni takbribani mwezi mmoja tokea kampuni hiyo ianze kuuza hisa zake katika soko la hisa nchini Marekani.
Kampuni ya Jumia iliorodheshwa katika soko la hisa la New York (Wall Street) huku ikichukua sifa nyingi – wawekezaji wakiipatia jina la utani la ‘Africa’s Amazon’, yaani Amazon ya Afrika. Ukiwa na mlinganisho na kampuni kubwa ya Marekani ya Amazon inayotoa huduma zinazofanana na Jumia, ikiunganisha wauzaji mbalimbali na wanunuaji bidhaa.
Bei ya hisa zake imeporoka kwa takribani asilimia 15 baada ya madai ya Citron kuwekwa wazi.
Habari nzuri zimeanza kugeuka mbaya baada ya shirika moja la data linalofuatiliwa na wawekezaji la Citron kutoa ripoti likisema kampuni ya Jumia imedanganya kwenye data za ukuaji wake na wateja wake ili kuwavutia wawekezaji.
Madai ya Citron;
- Jumia wameripoti idadi kubwa ya watumiaji kuliko uhalisia – ikiwa ni mlinganisho wa idadi iliyokuwa kwenye moja ya ripoti ya Jumia kwa wawekezaji wake wakuu (kabla ya kuingia kwenye mfumo wa hisa)
- Hisa za Jumia hazina thamani na kwamba wawekezaji wake watapata hasara tuu
Majibu ya Jumia;
Sacha Poignonnec mmoja wa waanzilishi wa kampuni hiyo apinga vikali
- Jumia imesema data za utumiaji wa huduma hiyo walizozitoa ni sahihi na hawatabadilisha
- Ripoti hii ya Citron ni ya nia mbaya – kwani haina ukweli wowote bali inalenga kutengeneza wasiwasi kwa wawekezaji
- Jumia wamesema utofauti wa namba unaweza ukawa ni wa kitofauti kulingana na muda na walengwa wa ripoti husika.
Andrew Left wa Citron amekaririwa na chombo cha habari cha FT akisema anakaribisha Jumia waende kutoa malalamiko ya kisheria kwani atakuwa mwenye furaha kwenda kushindana nao kupitia ofisi ya usimamizi wa biashara za hisa ya Marekani.