Mawe kadha wa kadha yameshawahi kupita karibu na uso wa dunia lakini jiwe Florence ni kubwa kuliko yote yaliyowahi kupita karibu na sayari yetu.
Kitendo cha jiwe hili kupita karibu na dunia kinatokea karibu karne moja iliyopita na linatarajiwa kupita umbali wa takribani milioni 7. Jiwe la Florence linakadiriwa kuwa na kipenyo (diameter) cha kilometa 4.4.
Wanasayansi wa anga wanasema ingawa ni kubwa sana na ambalo linaweza kuleta madhara makubwa kama likigongana na sayari, watu waondoe hofu. Jiwe hilo halina hatari yoyote kwetu kwa sasa, LABDA karne nyingi sana huko mbeleni. 🙂
Jiwe la Florence – lililogundulika mnamo mwaka 1981; linaweza kuwa mara 18 ya wastani wa umbali kati ya Dunia na Mwezi. Ni jiwe kubwa kubwa zaidi kuwahi kupita karibu na dunia yetu tangu kuanzishwa kwa mpango wa shirika la anga za mbali la Marekani NASA, katika mpango wa kuchunguza na kubaini mawe yaliyopo karibu na sayari Dunia.
Kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2017 Florence ni jiwe la angani lililopo kwa kukadiria tangu mwaka 1890 na ukaribu huo hautawahi kutokea hadi baada miaka 2500.
Kitu chenye ukubwa wa jiwe Florence kinaweza kuleta athari kubwa kama kikigonga Dunia. Wanasayansi wanaamini kuwa sasa wamebaini zaidi ya 90% ya miamba ya aina hiyo ya kutisha inayopita angani karibu na sayari yetu.
Chanzo: BBC