Kampuni ya Apple imetoa mwaliko kwa waandishi wa habari za teknolojia na wadau mbalimbali wa tasnia hiyo kuhudhuria tukio maalum katika ukumbi wa Steve Jobs Theater huko Cupertino, California siku ya Jumatano tarehe 12 Septemba 2018.
Siku hiyo inatarajiwa kuambatana na kutangazwa simu mpya za iPhone 9 na iPhone 11 au iPhone X Plus. Hata hivyo, majina ya simu hizo bado hayajathibitishwa kuwa ndio majina rasmi ila taarifa zinasema huenda zikazinduliwa simu tatu.
Tetesi zinasema kwamba iPhone X itakuwa na kioo cha ukubwa inchi 5.8, iPhone 11 itakuwa na inchi 6.5 na iPhone 9 inchi 6.1.
Pia bado haijajulikana sifa halisi ya simu zitakazozinduliwa ingawa kuna taarifa za tetesi kuhusiana na matoleo hayo mapya.