Halotel kupitia HaloPesa wameendelea kufikiria siku hadi siku ili kufikia lengo na sasa kuna huduma ya vifurushi maalum.
Karibu kila kapuni ya mtandao wa simu nchini Tanzania una kadi za simu aina mbali; zile za kawaida na nyingine zinakuwa na upendeleo wa aina yake maarufu kama “Laini ya mwanachuo”.
Ilikuwa ni jambo ambalo limeshazoeleka kuwa kwa wenye kadi za simu (Halotel) ambazo si za chuo basi wao hawawezi kufaidi vifurushi hivyo vya kipekee lakini hilo limebadilika isipokuwa tu itakubidi utumie HaloPesa kuweza kununua kifurushi cha chuo.