Huawei yakiri kutoipita Samsung mwaka huu. Lengo la kampuni ya Huawei la kuipiku Samsung kwa mwaka huu na kuwa namba moja duniani kwa mauzo ya simu, limeonekana kuingia dosari baada ya kuwekewa vikwazo na serikali ya Marekani.
Uongozi wa Huawei umekubali sasa itachukua muda mrefu kuliko ilivyo tarajiwa kuja kuipiku Samsung kutoka namba moja katika mauzo ya simu.
Akizungumza Afisa wa kimkakati wa Consumer Business Group, Bwana Shao Yang alisema itakuwa ngumu kwa Huawei kuipiku Samsung katika robo ya nne ya 2019 kufuatia zuio la biashara ndani ya marekani.
Alisema Huawei imeuza simu takribani 500,000 hadi 600,000 kwa mwanzoni mwa mwaka, na ilitarajiwa kuuza simu kati ya 101 milioni hadi 121 mwishoni mwa mwaka huu.
Lakini kufuatia kuzuiwa kuuza simu zake ndani ya Marekani na zuio la kutotumia kwa huduma za Google kama Play Store kumeathiri na kutaathiri kwa kiasi kikubwa soko la simu hizo hususani nje ya soko la China na hasa hasa ikiwa barani Ulaya.